MAN UNITED KUFANYIWA UMAFIA MKUBWA NA REAL MADRID - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, November 23, 2018

MAN UNITED KUFANYIWA UMAFIA MKUBWA NA REAL MADRID

HABARI KUU

Mshambuliaji wa England Marcus Rashford, mwenye umri wa miaka 21, yupo tayari kujadiliana na Real Madrid iwapo hatofanikiwa kujumuishwa katika orodha ya kwanza ya timu ya Manchester United. (Sun)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anasema hana wasiwasi kuhusu mkataba wa Christian Eriksen na anasisitiza klabu hiyo 'inawajibika' kumpatia mchezaji huyo wa kiungo cha kati raia wa Denmark mkataba mpya wa muda mrefu. (Standard)

Timu ya kiwango cha juu ya Uturuki Sivasspor imewasiliana na mshindi mara nane wa mbio fupi katika Olimpiki, Usain Bolt katika kinachowezekana kuwa ni mkataba wa nusu ya pili katika msimu.(TRT World)

Manchester United inaamini Jose Mourinho ameepuka uasi wa wachezaji Old Trafford. (Standard)

Juventus inatafakari kumsajili mchezaji wa kiungo cha kati wa Wolves na timu ya taifa ya Ureno, Ruben Neves, mwenye umri wa miaka 21, ifikapo Januari. (Tuttosport)

Manchester United inatuma maafisa kwenda kumwinda mlinzi wa Fiorentina Nikola Milenkovic, mwenye miaka 21, atakapocheza dhidi ya Bologna Jumapili. (Mail)

Mkuu wa Newcastle Rafa Benitez anataka kumsajili mshambuliaji wa Atlanta United Miguel Almiron. West Ham na Everton pia wana hamu ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Paraguay mwenye thamani ya £15m. (Sun)

Kocha mkuu wa Watford Javi Gracia atasaini mkataba mpya katika klabu hiyo wiki ijayo utakaomfikisha hadi mwisho wa kampeni ya mwaka 2020-21. (Sky Sports)

Winga Mohamed Salah, mwenye umri wa miaka 26, huenda akaondoka Liverpool "katika msimu mmoja au miwili" iwapo klabu hiyo itashindwa kunyanyua taji, kwa mujibu wa kocha wa Misri Javier Aguirre. (ONSport kupitia Goal.com)

Kipa wa Burnley na timu ya taifa England Tom Heaton, mwenye miaka 32, ana hamu ya kuhamia Leeds United. (Talksport)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Inter Milan Radja Nainggolan, mwenye umri wa miaka 30, amesema hana majuto kuhusu kukataa uhamisho kwenda katika ligi kuu England. Mchezaji huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Ubelgiji alihusishwa na uhamisho kwenda Chelsea na Manchester United. (ESPN)

Crystal Palace na West Ham wana hamu ya kumsajili mchezaji mwenye umri wa miaka 30 wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ujerumani Sandro Wagner, lakini timu hizo mbili katika ligi ya Primia zinakabiliwa na ushindani kutoka Galatasaray na klabu nyingine katika ligi ya Ujerumani Bundesliga. (Bild)

AC Milan ina hamu ya kumsajili beki wa kati wa Atletico Madrid na mchezaji timu ya taifa ya Uruguay Diego Godin, ambaye yupo huru katika msimu wa joto ujao.(Corriere dello Sport)

Aliyekuwa mchezaji wa kiungo cha kati wa England Scott Parker, mwenye umri wa miaka 38, atakuwa naibu meneja wa Claudio Ranieri huko Fulham. (Football.London)

Uganda wafuzu kushiriki kombe la AFCON 2019
Stoke inapanga uhamisho wenye thamani ya £5m kwa mshambuliaji mwenye umri wa miaka 22 wa Birmingham Che Adams ifikapo Januari. (Telegraph)

Aston Villa inatafakari kumuita kwa mara nyingine kipa wa England Jed Steer, mwenye miaka 26, kutoka mkataba wake wa mkopo huko Charlton Athletic ifikapo Januari. (Birmingham Mail)

Bora za Alhamisi
Nahodha wa zamani wa Manchester United Paul Ince anasema itafaidi pande zote ikiwa kiungo wa kati Mfaransa Paul Pogba, 25, ataondoka Januari. (Paddy Power, via Express)

Image caption
Paul Pogba
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola anahisi huenda akaongoza kandanda ya kimataifa hivi karibuni. (Telegraph - subscription required)

Barcelona wanataka mshambulizi raia wa Brazil Neymar, 26, kumaliza uwepo wake huko Paris St-Germain na kutafuta njia ya kurudi huko Nou Camp. (Goal)

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 20.11.2018
Kiungo wa kati wa Stoke Charlie Adam, 32, hajakana kurudi Rangers kujiunga na mchezaji mwenzake huko Liverpool Steven Gerrard. (Talksport, via Express)

Wing'a wa miaka 20 wa Borussia raia wa Marekani Christian Pulisic amehusishwa na kuhama kwenda Liverpool na anaamini kuwa meneja Jurgen Klopp na meneja ambaye wachezaji wote wangependa kumchezea. (Liverpool Echo)

Mshambuliaji wa Newcastle United raia wa Uingereza Dwight Gayle, 28, anafuta mkataba wa kudumu kwenda West Brom msimu ujao. (Northern Echo)

Mshambuliaji wa Liverpool raia wa Ubelgiji Divock Origi, 23, na mlinzi wa zamani wa Cameroon Joel Matip, 27, watahamia Uturuki mwezi Januari. Galatasaray wanamtaka Origi huku Matip akilengwa na Fernerbahce.

Kuhama kwa mchezaji wa miaka 20 wa River Plate kiungo wa kati raia wa Argentina Exequiel Palacios kwenda Real Madrid kwa kima cha pauni milioni 22.3 kutathibitishwa baada ya fainali za Copa Libertadores (Goal)

Kutoka BBC

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI