AJIBU KUWAUMIZA SIMBA KWA UJANJA HUU - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, November 21, 2018

AJIBU KUWAUMIZA SIMBA KWA UJANJA HUU

HABARI KUU

Nyota wa timu ya Yanga, Ibrahimu Ajibu amesema kuwa ataendeleza rekodi yake ya kufanya maajabu awapo uwanjani kwa kuwa muda wa kuisaidia timu ni sasa.

Ajibu amefanikiwa kuhusika katika mabao 12 kati ya 17 ambayo Yanga wamefunga kwenye michezo 10 waliyocheza.


"Kazi yetu kubwa ni kuhakikisha matokeo yanapatikana, kila nikipata nafasi ni lazima niitumie ipasavyo kwani nafanya kazi kwa ajili ya timu yangu.


"Ushirikiano uliopo ndani ya timu unatujenga na kufanya tuwe katika hali ya furaha muda wote, hivyo tupo tayari kwa ajili ya kupata matokeo," alisema.


Mwadui FC wataikaribisha Yanga kesho kwenye uwanja wa Kambarage huku rekodi zikionyesha kuwa Yanga hajapoteza mchezo hata mmoja kati ya 10 aliyocheza huku Mwadui FC akiwa amepoteza michezo 6 kati ya 13 aliyocheza.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI