Kocha Yanga kuhusu kiwango cha Kamusoko vs Kagera Sugar - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, March 10, 2018

Kocha Yanga kuhusu kiwango cha Kamusoko vs Kagera Sugar

HABARI KUU
Kiungo wa kimataifa wa Zimbabwe Thabani Kamusoko alirejea uwanjani kwenye mechi ya Yanga dhidi ya Kagera Sugar baada ya kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na kuuguza majera.
Kamusoko hakuonekana uwanjani tangu alipoumia Septemba 16, 2017 kwenye mchezo wa ligi kati ya Majimaji dhidi ya Yanga, katika mechi dhidi ya Kagera Sugar alicheza kwa dakika 71 kabla ya kupumzishwa kumpisha Yusuph Mhilu.
Kocha msaidizi wa Yanga Shadrack Nsajigwa amesema benchi la ufundi limeridhishwa kwa kiwango alichokionesha Kamusoko licha ya kuwa nje kwa muda mrefu.
“Ni mchezaji ambaye anakiwango kizuri siku zote lakini kwa vile ametoka kwenye majeraha tunaona anaendelea vizuri ndio maana tumeanza kumpa mechi na tumeridhika kwa dakika ambazo tulipanga acheze halafu tukampumzisha.”

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI