Jaji Mkuu awataka wananchi kuchukua hatua dhidi ya maofisa wanaojihusisha na rushwa - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, January 28, 2018

Jaji Mkuu awataka wananchi kuchukua hatua dhidi ya maofisa wanaojihusisha na rushwa

HABARI KUU
jajiJaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amewataka wananchi kuchukua hatua dhidi ya maofisa wa Mahakama wanaokiuka maadili ya kazi na wanaojihusisha na vitendo vya rushwa badala ya kulalamika.

Pia, ametaka wananchi kutambua  wanapokwenda mahakamani si lazima washinde ndipo waone haki imetendeka kwa kuwa uamuzi wa Mahakama ni mchakato unaopitia mtiririko maalumu.

Profesa Juma amesema hayo leo Jumapili Januari 28,2018 alipozindua Wiki ya Sheria katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

“Mahakama inawathamini wananchi. Tumeweka matangazo kwenye ngazi mbalimbali za Mahakama ambayo yanaonyesha namba za simu za wote wanaohusika,” amesema.

Profesa Juma amesema, “Kama mwananchi akiona hatendewi haki labda anaombwa rushwa, badala ya kulalamika tu atumie namba zile za simu kupiga kwa mamlaka husika, hasa Takukuru (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa) ambao ndio wanahusika na suala hilo.”

Alisema, “Mwananchi akiwa analalamika tu bila kuchukua hatua hawezi kuisaidia Mahakama, kwa hiyo waanze kuchukua hatua.”

Amewataka watumishi wa Mahakama na watoa haki kuwa na maadili mema na kutojihusisha na vitendo vya rushwa ili wananchi wawe na imani na Mahakama.

Jaji mkuu amesema kumekuwa na dhana kuwa mtu anapokwenda mahakamani ni lazima ashinde ndipo anaona kuwa haki imetendeka.

Amesema ili haki ipatikane kuna mlolongo wa hatua na utaratibu wa kufuata na la msingi ni mtu kusikilizwa ndipo Mahakama inatoa uamuzi.

“Sasa maamuzi yanayotoka si lazima wewe ushinde, huo ndio msingi wa haki. Wananchi wengi wanadhani kwamba wakienda mahakamani ni lazima tu washinde,” amesema.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI