Rais wa kikee wa pekee Afrika aendelea kushinikizwa ajiuzulu - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, March 18, 2018

Rais wa kikee wa pekee Afrika aendelea kushinikizwa ajiuzulu

HABARI KUUBi.Gurib-Fakim amekuwa akituhumiwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha.Bi.Gurib-Fakim amekuwa akituhumiwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha.
Rais pekee wa kike barani Afrika, rais wa Mauritius, Ameenah Gurib-Fakim angali anakabiliwa na shinikizo kwamba ajiuzulu.
Bi.Gurib-Fakim amekuwa akituhumiwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha.
Bi.Gurib amekuwa akikanusha madai hayo ya kutumia kiasi kikubwa cha fedha kutoka shirika lisilo la kiserikali fedha ambazo zilinuiwa kusaidia katika ada za wanafumzi kutoka jamii maskini.
Anasemekana alizitumia kwa ajili ya matumizi yake binafsi ya nguo na vitu vingine vya thamani.
Lakini siku moja baada ya kukataa wazo la kujiuzulu wakili wake Yusuf Mohamed aliwaambia waandishi wa habari wa nchi hiyo kuwa rais huyo huenda atajiuzulu.
Waziri mkuu wa nchi hiyo alisema rais huyo angeachia wadhifa wake Jumatatu iliyopita, jambo ambalo halikufanikishwa .
Bi Gurib amekuwa akisema fedha hizo alizirudisha na hivyo hana kosa lolote.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI