SANKHANI MKANDAWIRE AWAVURUGA MBEYA CITY, ASAINI MIAKA MIWILI MALAWI NA HUKU ANA MKATABA HADI MWAKANI - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, January 27, 2018

SANKHANI MKANDAWIRE AWAVURUGA MBEYA CITY, ASAINI MIAKA MIWILI MALAWI NA HUKU ANA MKATABA HADI MWAKANI

HABARI KUU
 

Sankhani ‘Mkango Plus’ Mkandawire (kulia) akisaini mkataba wa kurejea Big Bullets nchini Malawi juzi 
Amesema wakati anajiunga na Mbeya City Juni mwaka juzi alisaini mkataba wa miaka mitatu ambao unamalizika Juni mwakani.
 
Kimbe alisema mchezaji huyo aliondoka wiki iliyopita akiomba ruhusa anakwenda kwao kuna msiba na akaahidi kurejea Jumatatu ya Januari 29.
 
Na kuhusu madai kwamba mchezaji huyo ameamua kuvunja mkataba kwa sababu hajapewa mishahara ya miezi mitano Mbeya City, Kimbe amesema ni kweli. 
 
“Si kweli. Sankhani anadai mshahara wa mwezi mmoja tu huu tulionao wa kwanza. Mshahara wa Desemba (2017) ulichelewa ukatoka wakati amekwenda Malawi na amewekewa. Tuseme mikononi mwetu kuna mishahara yake ya miezi miwili,”amesema Kimbe.
 
Zaidi ya hapo, Kimbe amesema kwamba Sankhani pia anadai sehemu ya ada ya kusaini ambayo katika makubalino ya mkataba wa miaka mitatu ni awe anapewa kwa awamu, jambo ambalo hata mchezaji mwenyewe analielewa.
 
“Sisi tumeona hizo nakala za magazeti na tunazo kama ushahidi. Tunasubiri ruhusa yake iishe (Jumatatu), asipotokea tunaandika barua TFF (Shirikisho la Soka Tanzania) na FIFA (Shirikisho la Soka la Kimataifa) kuwashitaki klabu na mchezaji mwenyewe,”amesema Kimbe.
 
Nchini Malawi, magazeti mbalimbali yameripoti Mkandawire amerejea Nyasa Big Bullets kwa kusaini mkataba wa miaka miwili akitokea Mbeya FC alikodumu kwa miaka miwili.
 
Mkandawire amesaini kwa ada Kwacha Milioni 2 na mshahara wa Kwacha 250 000 kwa mwezi akiungana na wachezaji wengine wapya waliosajiliwa mwezi huu, Righteous Banda kutoka Civil Sporting Club, Patrick Phiri kutoka Premier Bet Wizards na Precious Phiri kutoka Azam Tigers.
 
The Nation limeandika mchezaji huyo amesema kwamba amevunja mkataba na Mbeya City kwa makubalino na klabu hiyo.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI