Mashindano ya urembo wa ngamia Saudi Arabia yatumbukia katika kashfa - NURU YA HABARI TZ

KWA HABARI ZA UHAKIKA ZA KITAIFA NA KIMATAIFA


HABARI MPYA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, January 29, 2018

Mashindano ya urembo wa ngamia Saudi Arabia yatumbukia katika kashfa

HABARI KUU
 A man cheers as he rides a camel during King Abdulaziz Camel Festival in Rimah Governorate, north-east of Riyadh, Saudi Arabia January 19, 2018

Ngamia 12 wamepoteza sifa za mashindano ya urembo nchini Saudi Arabia baada ya wamiliki wao kuwachoma sindano ya kubadili maumbile.

Maelfu ya ngamia wameshirikiswa katika tamasha la Mfalme Abdulaziz na kushindanishwa kwa muonekano wa nyuso zao, nundu na maumbile yao.

Lakini majaji waliingia kati wakati walipogundua kwamba baadhi ya udanganyifu ulifanyika na baadhi ya wamiliki waliotaka kushinda tuzo za fedha.
Saudi men stand next to camels as they participate in King Abdulaziz Camel Festival in Rimah Governorate, north-east of Riyadh, Saudi Arabia January 19, 2018

Vile vile tamasha hilo lina mashindano ya riadha ya ngamia na kuonja maziwa, lina tuzo ya fedha taslim dola milioni 57.

Mtandao wa habari wa The National imeripoti kuwa Ali Al Mazrouei, mwana wa mfugaji bingwa , alisema dawa ya botox ilitumika kwenye midomo, pua na hata taya.

"Dawa hiyo inavimbisha kichwa kwa hio ukimuona ngamia unadhani ana kichwa,mdomo na pua kubwa" aliezea Mazrouei.
 A Saudi man walks in front of camels as he participates in the King Abdulaziz Camel Festival in Rimah Governorate, north-east of Riyadh, Saudi Arabia January 19, 2018















Majaji pia walikuwa wakishindanisha nundu na misuli ya ngamia.
Kabla ya tamasha hilo, vyombo vya habari vya Saudia viliripoti daktari wa wanyama alikamatwa akiwa pasua ngamia hao ili kuwabadilisha ukubwa wa masikio pamoja na kuwachoma sindano ya dawa ya kubadilisha maumbile.

Jaji mkuu Fawzan al-Madi amesema kuwa ngamia ni moja wapo wa "nembo ya Saudi Arabi"
Mashindano hayo ya urembo wa ngamia yalifanyika kwa mara ya kwanza mwaka 2000.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

HABARI